Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Hatma ya Matangazo Mubashara Kesi ya Tundu Lissu Kujulikana Agosti 18 – Video

  • 3
Scroll Down To Discover

Wakili wa utetezi, Dkt. Rugemeleza Nshala, amesema bado haijajulikana iwapo kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, itarushwa moja kwa moja (mubashara) au la.

Akizungumza baada ya kikao cha mahakama, Dkt. Nshala alifafanua kuwa uamuzi wa urushaji mubashara utabainika baada ya kikao kinachotarajiwa kufanyika Agosti 18, 2025, kufuatia kuahirishwa kwa shauri hilo.

Kesi hiyo, inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Franco Kiswaga, imezua mjadala mkali baada ya upande wa mashtaka kuomba matangazo ya mubashara yasitishwe. Sababu kuu iliyotolewa ni kulinda utambulisho wa mashahidi raia, hoja ambayo imepingwa vikali na upande wa utetezi.



Prev Post Salum Mwalimu: Sitajibizana na wanaonibeza, najikita kwenye kile Watanzania wanataka
Next Post DCEA Yakamata Tani 18.5 za Dawa Mpya ya Kulevya Zilizofichwa Kwenye Mifuko ya Mbolea
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook