

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Timu ya Simba na Yanga mara baada ya mazungumzo na Viongozi hao, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
tarehe 13 Juni, 2025.
Mazungumzo ya Rais Samia na Viongozi wa vilabu hivyo vikubwa, shindani na vikongwe nchini Tanzania, vikijizolea mamilioni ya mashabiki na wanachama yanakuka wakati huu ambao kumekuwa na mvutano mkubwa kuhusu Mchezo wao wa ligi kuu Tanzania bara ambapo kila mmoja amekuwa na msimamo wake suala ambalo limetatanisha uwepo wa mchezo wao Jumapili hii mara baada ya kuahirishwa kwa mchezo huo hapo awali.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!