
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Nchemba, leo Aprili 2, 2026 amesafiri kwa treni ya reli ya kisasa (SGR) akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya kikazi.
Katika safari hiyo, Dkt. Mwigulu ameambatana na mkewe, Mama Neema Mwigulu Nchemba, ambapo walionekana wakitumia huduma ya treni hiyo ya kisasa inayozidi kuimarisha usafiri wa haraka na salama nchini.
Safari ya SGR inaendelea kuwa chaguo muhimu kwa viongozi na wananchi kwa ujumla kutokana na ufanisi wake, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuboresha miundombinu ya usafiri na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.



The post Waziri Mkuu Mwigulu Asafiri kwa SGR Kutoka Dodoma Hadi Dar – Picha appeared first on Global Publishers.









Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!