
Gari la muziki lililokuwa kwenye msafara wa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema), John Heche limepata ajali alfajiri ya leo katika maeneo ya Msamvu, Morogoro.
Gari hilo lilikuwa likielekea Kivukoni – Ulanga, Igima – Mlimba, na Ifakara Mjini – Kilombero kwa ajili ya kuanza ziara kwenye mikoa hiyo.
Inaelezwa kuwa gari hilo lilikuwa likiendeshwa na Twaha Mwaipaya na waliopata ajali wamejeruhiwa na wamekimbizwa hospitalini kwa uangalizi zaidi wa kiafya.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!