Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Sheikh Ponda Ajiunga na ACT Wazalendo – (Picha +Video)

  • 24
Scroll Down To Discover


Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu (kulia), akiongea jambo na Sheikh Ponda (kushoto) kwa nyuma ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu.

Dar es Salaam, Juni 5, 2025 — Chama cha ACT Wazalendo leo Alhamisi Juni 5, 2025 kimempokea rasmi Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, aliyejiunga na chama hicho kama mwanachama mpya katika hafla iliyofanyika Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Sheikh Ponda, ambaye ni miongoni mwa viongozi wa dini ya Kiislamu wanaotambulika kwa ushawishi mkubwa nchini, alitangaza uamuzi wake wa kujiunga na ACT Wazalendo mbele ya umati wa wafuasi na viongozi wa chama hicho, akisema kuwa wakati umefika kwa viongozi wa dini kushiriki kikamilifu katika kupigania haki, usawa na maendeleo ya kweli ya wananchi.

“Nimeamua kujiunga na ACT Wazalendo kwa sababu ninayaona matumaini ya kweli ya mabadiliko ndani ya chama hiki. Tunahitaji siasa zenye maadili, zinazojali watu na zinazoweka mbele maslahi ya umma, si maslahi binafsi ya wachache,” alisema Sheikh Ponda wakati wa tukio hilo.



Prev Post Mama Ajifungua Watoto 3, Baba Amwaga Machozi Aomba Msaada – Video
Next Post Gari la Msafara wa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Wapata Ajali – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook