
Mbunge wa Jimbo la Nyasa, John Nchimbi, amechangia katika Kikao cha Tatu cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, leo Aprili 2, 2026 jijini Dodoma.
Katika mchango wake, Nchimbi amezungumzia sakata la mafuta linaloendelea kufuatia vita kati ya Israel na Iran, akitoa wito kwa watumishi wa umma kupunguza matumizi ya usafiri, hususan kuepuka kutumia magari binafsi kwa safari zisizo za lazima.
Amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza matumizi ya mafuta katika kipindi hiki ambacho bei imepanda kutokana na athari za mzozo huo wa kimataifa.
Mkutano huo wa Tatu wa Bunge umejikita katika kujadili utekelezaji wa bajeti za wizara kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
The post Video: Mbunge John Nchimbi Ajilipua Sakata la Mafuta, Watumishi Wanaotumia Magari Binafsi appeared first on Global Publishers.











Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!