Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia akutana na viongozi wa TUCTA Ikulu ya Dar

  • 6
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 12, 2025, amekutana na viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika Ikulu ya Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, viongozi wa TUCTA wamempongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kutekeleza ahadi alizozitoa, ikiwemo nyongeza ya mishahara, kupandisha madaraja ya watumishi wa umma na kuboresha mazingira ya kazi nchini.

Viongozi hao wamesema hatua hizo zimeongeza ari ya wafanyakazi na kuimarisha ustawi wa maisha yao, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na serikali katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa.

 



Prev Post Mwalimu aapa kuleta mabadiliko baada ya kuchukua fomu ya Urais
Next Post Mahakama Kuu yatupilia mbali pingamizi la Lissu dhidi ya mashahidi wa siri – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook