

Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids ameweka wazi kuwa wana mchezo mmoja mkononi ambao wakishinda watakuwa mabingwa.
Mchezo huo ni dhidi ya Yanga SC ambao unatarajiwa kuchezwa Juni 25 2025, Uwanja wa Mkapa ikiwa ni mzunguko wa pili msimu wa 2024/25.
Simba SC katika mchezo wa raundi ya 30 ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar likifungwa na Steven Mukwala inafikisha pointi 78 nafasi ya pili na vinara ni Yanga SC wenye pointi 79.

Fadlu amesema walipata kazi kubwa mbele ya Kagera Sugar hivyo mchezo mmoja uliobaki wakishinda watakuwa mabingwa wa ligi kuu ambayo ni namba nne kwa ubora Afrika.
“Tumepata pointi tatu mbele ya Kagera Sugar unaona haukuwa mchezo mwepesi kwetu, tuna mchezo mmoja ambao tukishinda tutakuwa mabingwa.”
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!