
Mama mzazi wa binti aliyedanganywa na dereva bodaboda kwa ahadi ya shilingi laki 3 kwa ajili ya matibabu, na hatimaye kubeba ujauzito bila msaada, amefunguka juu ya mateso makubwa yanayoikumba familia yake.
Mama huyo, ambaye alipata upofu na kutelekezwa na mumewe, amesema maisha yao yamekuwa ya mateso makubwa. Anaishi kwenye mazingira magumu na binti yake ambaye sasa ni mjamzito wa miezi 6 baada ya kudanganywa na dereva bodaboda aliyemtelekeza.
Kwa uchungu, mama huyo ameomba Watanzania wenye mapenzi mema wamsaidie kupata pesa za matibabu ya macho yake, kwani anapitia maumivu makali kila siku. Pia, ameomba msaada kwa ajili ya binti yake ili aweze kupata msaada wa kifedha na kihisia katika changamoto anazopitia.
Kwa yeyote aliyeguswa, unaweza kutoa msaada kupitia namba:
0679 734 392 (Asia Rashid)
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!