Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Katazo la Trump Lawakwamisha Wahamiaji Kutoka Haiti na Mataifa 11 Mengine

  • 24
Scroll Down To Discover

Kuanzia Jumatatu, agizo jipya la Rais wa Marekani, Donald Trump, linaanza kutekelezwa rasmi, likiwaathiri raia kutoka nchi 12, wakiwemo watu wa Haiti ambao tayari wanapitia hali ngumu ya kiusalama na kibinadamu.

Haiti, taifa linalokabiliwa na wimbi la uhalifu na linalotegemea misaada ya kimataifa, linaonekana kupokea pigo kubwa kutokana na mabadiliko haya ambayo yanakata fursa za kuungana na familia au kuendeleza biashara katika Marekani.

Elvanise Louis-Juste, raia wa Marekani mwenye asili ya Kihaiti aliyekuwa uwanja wa ndege wa Newark akielekea Florida, alisema hali ya Haiti si salama tena.

“Kuna utekaji nyara, mauaji—hali ni mbaya sana. Watu wanatafuta nafasi ya kuishi maisha ya kawaida,”alisema.

“Nina familia Haiti, na ukweli ni kwamba hali inakatisha tamaa.”

Mabadiliko haya hayabatilishi visa zilizotolewa awali, lakini kwa waombaji wapya, ombi litakataliwa isipokuwa kwa wale watakaotimiza masharti maalum ya kipekee.

Huko Haiti, hakuna harakati za wazi kuelekea Marekani, huku abiria wakiepuka kuzungumza na vyombo vya habari kwa hofu ya kulengwa baada ya kufika Marekani.

Wiki iliyopita, raia wengi wa Haiti walijitokeza kwenye mitandao ya kijamii na redio wakionyesha hasira zao, huku baadhi wakimtuhumu Rais Trump kwa ubaguzi.

Mbali na Haiti, nchi nyingine zilizotajwa ni pamoja na Afghanistan, Myanmar, Chad, Jamhuri ya Kongo, Guinea ya Ikweta, Eritrea, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen.

Wataalamu wa uhamiaji wanasema hatua hii mpya imeundwa kwa makini ili kuepusha changamoto za kisheria zilizowahi kuibuka kwenye agizo la awali la Trump, na safari hii inalenga mchakato wa maombi ya visa moja kwa moja.




Prev Post Makalla: Kauli ya No Reforms Haizuii Wala Kuahirisha Uchaguzi Mkuu
Next Post Diamond Platnumz feat Bien – Katam (Official Lyric Audio)
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook