
FAINALI ya Kombe la Shirikisho la CRDB kati ya Yanga dhidi ya Singida Black Stars imepangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Amaan huko Unguja, Zanzibar.
Mchezo unatarajiwa kupigwa Juni 28, mwaka huu huko Zanzibar ambako timu hizo mara ya mwisho kukutana kwenye uwanja huo katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara mchezo uliomalizika kwa Yanga kushinda bao 1-0 lililofungwa na Pacome Zouzoua.
Yanga imefuzu kucheza fainali hiyo baada ya kuwaondoa JKT Tanzania katika mchezo wa nusu huku Singida Black Stars ikiwaondoa Simba.
Stori na Wilbert Moland, GPL
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!