Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

BoT yasitisha uuzaji wa dhahabu kufuatia kushuka kwa bei duniani

  • 13
Scroll Down To Discover

Banki Kuu ya Tanzania (BoT) imesitisha kwa muda mpango wake wa kuuza dhahabu kutokana na kushuka kwa bei ya dhahabu katika soko la dunia, hatua inayolenga kulinda thamani ya akiba hiyo wakati hali ya soko ikiwa haijatulia.

Kwa mujibu wa BoT, hadi Machi 2026 benki hiyo ilikuwa na takribani tani 19.6 za dhahabu, karibu kufikia lengo la tani 20, huku ikikusanya kwa kasi dhahabu tangu Oktoba 2024 ili kuimarisha akiba ya fedha za kigeni.

Akizungumza na gazeti la The Citizen, Gavana wa BoT, Emmanuel Tutuba, amesema si wakati mzuri kuuza dhahabu wakati bei zinashuka, akieleza kuwa benki hiyo itaendelea kufuatilia mwenendo wa soko na inaweza kuuza endapo bei zitapanda tena.

Uamuzi wa kusitisha mauzo umetokana na bei ya dhahabu kushuka baada ya kupanda kwa kiwango kikubwa mwanzoni mwa mwaka, ambapo iliwahi kuvuka dola za Kimarekani 5,000 kwa wakia lakini baadaye kushuka hadi takribani dola 4,555 kufikia Machi 31, 2026.

The post BoT yasitisha uuzaji wa dhahabu kufuatia kushuka kwa bei duniani appeared first on SwahiliTimes.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABRARI KATIKA MAGAZETI YA LEO APRILI 02, 2026
Next Post WAZIRI PROF. SHEMDOE AWASILISHA RANDAMA YA BAJETI OFISI YA WAZIRI MKUU
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook