
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya mazungumzo na viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Fedha pamoja na Taasisi ya Usafirishaji wa Bima ya Mikopo (KUKE) kutoka nchini Poland ofisini kwa Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma leo Februari 4, 2026.

Viongozi hao wamejadili kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR kipande cha 3 na 4) pamoja na kujadili fursa za kuimarisha ushirikiano wa kifedha baina ya Tanzania na Serikali ya Poland.

The post Waziri Mkuu Afanya Mazungumzo Na Waziri Wa Mambo Ya Nje Fedha Na Taasisi Ya Kuke Ya Poland appeared first on Global Publishers.






Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!