Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Man United Yakubaliana na Michael Carrick Kuwa Kocha Mkuu wa Muda

  • 24
Scroll Down To Discover

Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano ya mdomo na Michael Carrick kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Kocha Mkuu wa muda hadi mwisho wa msimu.

Makubaliano hayo yanakuja kufuatia mabadiliko ya benchi la ufundi katika klabu hiyo yenye maskani yake Old Trafford.

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa, Carrick ambaye ni mchezaji wa zamani wa Manchester United na amekuwa sehemu ya benchi la ufundi kwa muda, amepewa jukumu la kuiongoza timu wakati klabu ikiendelea na mchakato wa kumpata Kocha wa kudumu.

Uongozi wa Manchester United unaamini uzoefu wa Carrick ndani ya klabu, pamoja na uelewa wake wa falsafa na wachezaji, utasaidia kudumisha utulivu na ushindani wa timu katika mashindano yanayoendelea hadi msimu utakapomalizika.

Mashabiki wa klabu hiyo wanasubiri kwa hamu kuona mwelekeo wa timu chini ya uongozi wa Carrick, huku matarajio yakiwa ni kurejea kwenye matokeo mazuri na kuimarisha nafasi ya klabu hiyo katika ligi na mashindano ya kimataifa.

The post Man United Yakubaliana na Michael Carrick Kuwa Kocha Mkuu wa Muda appeared first on Global Publishers.



Prev Post Kampeni za uchaguzi zapamba moto Uganda. Katika Dira ya Dunia TV
Next Post Serikali ya Uganda Yazima Intaneti Kuelekea Uchaguzi Mkuu
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook