Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Trump Aendeleza Mvutano na Ilhan Omar, Atupa Madai Mapya Yenye Utata

  • 53
Scroll Down To Discover

Rais wa Marekani wa zamani, Donald Trump, ameendelea kumkosoa Mbunge wa Bunge la Marekani, Ilhan Omar, ambaye ni raia wa Marekani mwenye asili ya Somalia.

Katika hotuba yake ya karibuni, Trump alirudia tuhuma tata dhidi ya Ilhan Omar, akidai kwamba aliolewa na kaka yake ili kupata uraia wa Marekani madhara ambayo Ilhan Omar amewahi kuyakana hadharani na ambayo hayajawahi kuthibitishwa na mamlaka yoyote.

Trump pia alimshutumu mbunge huyo kwa kutumia Katiba ya Marekani kuwasilisha madai na misimamo yake ya kisiasa, huku akirejea changamoto za kiusalama nchini Somalia kama sehemu ya hoja zake.

Kwa upande wake, Ilhan Omar katika matamko yake ya nyuma amesema mashambulizi ya Trump yanachochewa na chuki dhidi ya wahamiaji na Waislamu, akisisitiza kuwa kauli kama hizo huwa zinagawanya taifa.

Kauli hizo za Trump zimeibua mjadala mpana nchini Marekani, huku wachambuzi wa siasa wakizitaja kama sehemu ya mvutano wa muda mrefu kati ya kambi za kisiasa, na pia jitihada zake za kuwasha hamasa kwa wafuasi wake.

The post Trump Aendeleza Mvutano na Ilhan Omar, Atupa Madai Mapya Yenye Utata appeared first on Global Publishers.



Prev Post Kwa nini maandamano ya Disemba 9 nchini Tanzania yalifeli? Katika Dira ya Dunia TV
Next Post Mkuu wa Mkoa wa Arusha Awaonya Wanaopanga Vurugu
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook