

Wizara ya Mambo ya Nje ya China imemwita balozi wake wa Japan nyumbani kwa sababu ya matamshi yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Japan Takaichi Sanae kuhusu uwezekano wa kutokea kwa mzozo juu ya Taiwan.
Takaichi alikiambia kikao cha Bunge la Chini wiki iliyopita kwamba uvamizi wa China huko Taiwan kunaweza kuchukuliwa kama “hali ya kutishia maisha”, na kusababisha Japani kuchukua hatua ya kijeshi.
Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa China Sun Weidong alisema Takaichi anapaswa kubatilisha matamshi yake “vinginevyo chochote kitakachotokea Japan itawajibika,” kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje huko Beijing.
Hata hivyo, Waziri Mkuu Takaichi, baadaye alisema matamshi hayo yalitolewa kwa dhana ya hali mbaya zaidi inayoweza kutokea na haibadilishi msimamo uliopo wa serikali.
Wizara ya China ilisema Sun iliita matamshi ya Takaichi kuwa “ya nia mbaya” na kunukuliwa kuwa kile alichosema Takaichi kinadhoofisha msingi wa kisiasa wa uhusiano wa China na Japan.











Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!