Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Bunge la Marekani Laidhinisha Mpango wa Kumaliza Shutdown

  • 73
Scroll Down To Discover

Bunge la Wawakilishi (House of Representatives) limeidhinisha rasmi pakiti mpya ya fedha yenye lengo la kumaliza mgogoro wa kifedha uliosababisha kusimama kwa shughuli za serikali (government shutdown), hali iliyokuwa ikiathiri sekta nyingi za umma nchini humo.

Kupitia kura zilizopigwa usiku wa kuamkia leo, wabunge wengi waliunga mkono mpango huo wa bajeti, unaolenga kufungua tena taasisi za serikali na kurejesha huduma muhimu kwa wananchi.

Mpango huo sasa unasubiri kutiwa saini na Rais Donald Trump, hatua itakayohitimisha rasmi kipindi cha sintofahamu kilichosababisha watumishi wa umma wengi kukosa mishahara na taasisi za serikali kushindwa kutoa huduma kwa muda.

Uamuzi huu unatarajiwa kuleta ahueni katika sekta ya uchumi na huduma za kijamii, hasa maeneo yaliyoathiriwa zaidi na kufungwa kwa muda kwa mashirika ya serikali.

“Tunarejesha serikali kwenye reli. Huduma lazima ziendelee, na wananchi wasihisi athari za migogoro ya kisiasa,” alisema mmoja wa wabunge wakati wa kikao hicho.

Kwa hatua hii, serikali ya Marekani inatarajiwa kuanza kutoa huduma zake kwa kawaida, huku macho yote yakielekezwa kwa Rais Trump kuona kama atautia saini mpango huo bila marekebisho zaidi.

WAZIRI MKUU MPYA MWIGULU NCHEMBA ANAPIGIWA KURA KUTHIBITISHWA na WABUNGE KABLA ya KUAPISHWA



Prev Post Daniel Sillo Baran Achaguliwa Naibu Spika wa Bunge la 13
Next Post Waziri Mkuu Mwigulu: Serikali Itatekeleza Miradi Inayogusa Maisha ya Wananchi -Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook