
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango, leo tarehe 17 Oktoba 2025 amewasili Nairobi nchini Kenya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mazishi ya Kitaifa ya Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya marehemu Raila Amolo Odinga.
Mazishi ya Kitaifa ya marehemu Raila Odinga yanatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Nyayo, Jijini Nairobi.
Makamu wa Rais ameambatana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!