Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Kilio cha Teddy: Baba Anatokwa na Wadudu Jichoni, Anahitaji Msaada wa Haraka

  • 15
Scroll Down To Discover

Msichana mmoja anayeitwa Teddy, mkazi wa Chang’ombe, jijini Dar es Salaam, anapitia kipindi kigumu cha kumuuguza baba yake mzazi ambaye ana tatizo kubwa la kiafya.

Upande mmoja wa jicho la baba huyo umelika kabisa na kuwa na kidonda kikubwa kinachotoa wadudu, hali inayosababisha maumivu makali na taharuki.

Kutokana na hali ngumu ya maisha na ukosefu wa fedha, Teddy hulazimika kumtunza na kumsafisha baba yake mwenyewe nyumbani, bila msaada wowote wa kitabibu.

Kwa sasa, wanahitaji kiasi cha Tsh 500,000 kwa ajili ya kufanya vipimo muhimu ikiwemo T-SCAN, vitakavyomwezesha kuanza tiba ya mionzi katika Hospitali ya Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Teddy amewaangukia Watanzania wenzake na watu wenye mapenzi mema kumsaidia ili kuokoa maisha ya baba yake. Kama umeguswa na hali hii, tafadhali changia chochote kupitia namba:

📞 0756 194 166 – Frank Anthony Lingwetu

Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Prev Post Majaliwa Aagiza Usimamiaji Na Udhibiti Wa Ubora Wa Elimu
Next Post Maelfu Wanufaika na Upasuaji wa Mifupa na Ubongo MOI Katika Kipindi cha Februari–Mei 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook