
MAGAZETI Ya Leo Alhamisi tarehe 19 June 2025
MAGAZETI Ya Leo Alhamisi tarehe 19 June 2025
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kimetaja changamoto kadhaa wanazokabiliana nazo ikigusia uhaba wa watumishi, mifumo kutosomana, mgawanyo na utekelezwaji wa majukumu.
Akizungumza katika Kongamano la Kitaifa la Tibal linalokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 60 ya chama hicho, Rais wa MAT, Dk Mugisha Nkoronko amesema kuwa Wizara ya Tamisemi na Wizara ya Afya kuna mgawanyo wa majukumu ambao unasumbua, hivyo MAT inashauri kuwe na muundo utakaowezesha zisomane.
Pia ameshauri uwekezaji ufanyike katika eneo la watumishi wa afya ili kuondoa upungufu uliopo wa asilimia 55.
Pamoja na hayo MAT imesema kuwa kuna shida na wasiwasi katika utekelezaji wa bima ya afya kwa wote, huku ikipongeza juhudi zilizofanyika, hata hivyo wamesema jitihada zaidi zinahitajika.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!