

Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam imemshukuru Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azan Zungu na kuahidi kumchukulia fomu kwenye uchaguzi ujao kwa kuwa yeye ndiye mlezi wa seneti hiyo na amejitoa kuhakikisha Idara ya vyuo vikuu inaimarika nchini.
Pia wamemwomba mgeni rasmi, Dk. Tulia Ackson kumtia moyo msaidizi wake huyo na kwamba wanavyuo watasimama naye katika uchaguzi na kuhakikisha anashinda kwa kishindo.
Wamesisitiza kuwa hawana shaka kuwa Dk. Tulia atabaki kuwa spika wa bunge na Zungu ataendelea kuwa msaidizi wake.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa seneti, Pascrates Mwemezi katika shukrani zake kwa mgeni rasmi.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!