
MAGAZETI ya Leo Jumapili 01 June 2025
MAGAZETI ya Leo Jumapili 01 June 2025
Usaili wa madereva 800 waliotuma maombi ya kazi katika Kampuni ya Usafirishaji ya Serikali ya Qatar (Mowasalat), umekamilika rasmi Mei 31, 2025, jijini Dar es Salaam, baada ya kufanyika kwa siku tano mfululizo katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Usaili huo ulikuwa sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Qatar katika sekta ya ajira, ukiwalenga Watanzania waliopo tayari kufanya kazi ya udereva nchini humo.
Akizungumza wakati wa kufunga zoezi hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kufungua fursa za ajira kwa Watanzania nje ya nchi.
“Kampuni ya Mowasalat imeonyesha imani kubwa kwa vijana wetu. Ushirikiano huu una manufaa makubwa kwa Taifa letu, si tu kwa kupunguza tatizo la ajira, bali pia kwa kuongeza mapato ya fedha za kigeni kupitia Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi,” amesema Ridhiwan.
Mwakilishi wa Mowasalat, Khalid Abdulhameed Al Reyahi amesema Qatar inakabiliwa na upungufu wa madereva wa mabasi na malori, hivyo Tanzania imeonekana kuwa miongoni mwa nchi zinazoweza kusaidia kutokana na kuwa na nguvu kazi yenye nidhamu na maadili ya kazi.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!