Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Ibada Maalum Ya Mazishi Ya Cleopa Msuya Yafanyika Usangi Kivindu, Kilimanjaro (Picha +Video)

  • 39
Scroll Down To Discover

Kilimanjaro, Mei 13, 2025 — Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro na mikoa ya jirani wamekusanyika leo katika Kanisa la KKKT Kristo Mchungaji Mwema, Dayosisi ya Mwanga, Jimbo la Kaskazini, Usharika wa Usangi Kivindu, kushiriki ibada maalumu ya mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya.

Viongozi wa Serikali, viongozi wa dini, na wawakilishi wa taasisi mbalimbali wamehudhuria ibada hiyo ambayo imefanyika kwa heshima kubwa kwa kiongozi huyo aliyelitumikia Taifa kwa muda mrefu.

Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiuingiza mwili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya, katika Kanisa la KKKT Kristo Mchungaji Mwema, Usharika wa Usangi Kivindu, Dayosisi ya Mwanga, Jimbo la Kaskazini, mkoani Kilimanjaro, leo Mei 13, 2025, kwa ajili ya ibada maalumu ya mazishi ya kiongozi huyo.

Msuya, aliyefariki dunia mapema wiki iliyopita, alikumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kisiasa nchini Tanzania. Katika hotuba zao, viongozi mbalimbali walieleza kuwa alisimama kama kiongozi shupavu, mzalendo na mpenda haki aliyeacha alama isiyofutika katika historia ya Taifa.

Ibada hiyo imeongozwa na Askofu Mkuu wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, akisisitiza juu ya umuhimu wa kuenzi amani, mshikamano, na maadili aliyoyaishi Hayati Msuya.

Mazishi yamefanyika katika makaburi ya familia yaliyopo Usangi Kivindu, ambako alizaliwa na kukulia.

Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiwa katika Kanisa la KKKT Kristo Mchungaji Mwema; Dayosisi ya Mwanga, Jimbo la Kaskazini, Usharika wa Usangi Kivindu, mkoani Kilimanjaro, leo Mei 13, 2025, kushiriki ibada maalumu ya mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya.
Waziri Mkuu mstaafu, John Malecela akishiriki ibada maalumu ya mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya.
Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Tluway Sumaye.
Viongozi mbalimbali wa Serikali wakishiriki ibada maalumu ya mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya.




Prev Post Polisi Dar Yataja Sababu za Kumkamata Amani Golugwa wa Chadema
Next Post Sikia Wasifu Wa Charles Hillary Wawagusa Wengi, Ameacha Mjane – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook