Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Tume ya Uchaguzi Yatangaza Majimbo Mapya 8 na Kubadili Majina ya Majimbo 12

  • 39
Scroll Down To Discover

Tume Huru ya Uchaguzi imetangaza mabadiliko makubwa ya kiutawala katika mipaka ya majimbo ya uchaguzi nchini, ikiwemo mabadiliko ya majina ya majimbo 12 na kuanzishwa kwa majimbo mapya 8.

Kwa mujibu wa taarifa ya tume, majimbo hayo mapya yameanzishwa kutokana na kugawanywa kwa baadhi ya majimbo yaliyokuwa na ukubwa mkubwa au ongezeko la watu, hatua inayolenga kuboresha uwakilishi wa wananchi.

Majimbo mapya yaliyoanzishwa ni kama ifuatavyo:

Majimbo Mapya ya Uchaguzi: Kivule lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Ukonga, Mkoa wa Dar es Salaam na Chamazi – lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Mbagala, Mkoa wa Dar es Salaam.

Mengine ni Mtumba lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Dodoma Mjini, Mkoa wa Dodoma, Uyole lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Mbeya Mjini, Mkoa wa Mbeya na Bariadi Mjini lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Bariadi, Mkoa wa Simiyu.

Pia lipo Katoro lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Busanda, Mkoa wa Geita, Chato Kusini lilioanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Chato, Mkoa wa Geita na Utwangi lililoanzishwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Solwa, Mkoa wa Shinyanga.

Tume imesema mabadiliko haya ni sehemu ya maboresho ya mipaka ya kiutawala ili kuhakikisha uwiano wa idadi ya watu kwenye majimbo ya uchaguzi na ufanisi wa uwakilishi wa wananchi bungeni. Na Elvan Stambuli GPL



Prev Post FUNGUA MILANGO YA BAHATI KWENYE GATES OF OLYMPIA – SLOTI MPYA YA KISASA KUTOKA MERIDIANBET.
Next Post Safiri Mpaka Msitu wa Wachawi na Sloti ya Fairy Forest!
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook