Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

DUBE AONYESHA NJAA MABAO, YANGA YAITANDIKA MUEMBE MAKUMBI 4-0

  • 5
Scroll Down To Discover

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Prince Dube, amerejea kwa kishindo uwanjani baada ya kupona majeraha, akionesha makali yake kwa kuiongoza timu hiyo kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Muembe Makumbi City katika michuano ya Kombe la Muungano.

Katika mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la New Amaan Complex visiwani Zanzibar, Yanga ilianza kwa kasi na kudhibiti mchezo tangu dakika za mwanzo, jambo lililowaweka wapinzani wao katika presha kubwa.

Dube alianza kuandika bao la kwanza dakika ya 17 akimalizia pasi safi kutoka kwa Okello, kabla ya Frank Assinki kuongeza la pili dakika ya 34 kufuatia pasi ya Shekhan.

Yanga iliendelea kushambulia kwa kasi na kufunga bao la tatu dakika ya 38 kupitia Shekhan Khamis, akihitimisha kipindi cha kwanza kwa ubora mkubwa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ile ile ambapo Dube alirudi tena kambani dakika ya 57 akifunga bao lake la pili katika mchezo huo, akimalizia pasi ya Edmund na kuhitimisha karamu ya mabao kwa Yanga.

Ushindi huo unaipa Yanga mwanzo mzuri katika michuano hiyo, huku kurejea kwa Dube kwenye kiwango bora kikiwa ni taarifa njema kwa benchi la ufundi na mashabiki wa timu hiyo kuelekea mechi zijazo.

The post DUBE AONYESHA NJAA MABAO, YANGA YAITANDIKA MUEMBE MAKUMBI 4-0 appeared first on Soka La Bongo.



Prev Post HATARI KUBWA YANGA, UTI WA MGONGO WATIKISWA
Related Posts
© Image Copyrights Title

SIMBA WAITAKA YANGA ZANZIBAR NA BARA

Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook