MSHAMBULIAJI wa YANGA Clement Mzize, anatarajiwa kufanyiwa upasuajiĀ kufuatia changamoto ya kiafya inayomkabili.
Taarifa za kufanyiwa upasuaji kwake zimewekwa wazi na aliyekuwa mtaalam wa masuala ya misuli na utimamu wa mwili wa Yanga, Seroto Sekhwela maarufu kwa jina la SK Seroto, aliyewapokea nchini Afrika Kusini.
Kupitia ujumbe wake, Sekhwela alionesha mshikamano na upendo kwa nyota huyo akisema:
āChuma hunoa chuma. Nimempokea mmoja wa wachezaji bora kabisa wa Tanzania pamoja na Dk. Moses Etutu, mchezaji kutoka klabu yangu ya zamani ya Afrika Mashariki, Yanga,
āSasa ni familia, na leo anaingia kufanyiwa upasuaji. Namtakia nguvu, mikono ya madaktari iwe salama na arejee haraka uwanjani. Tuko pamoja nawe,ā amesema.
Mzize alikuwa nje kwa muda mrefu akiuguza jeraha la goti, alipata nafuu na kurejea kwenye mazoezi ambapo alicheza dakika za mwishoni mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Far Rabat ya Morocco ugenini na baada yah apo hakuonekana tena ikielezwa kuwa bado hakuwa imara.
The post KINACHOMSIBU MZIZE HUKO YANGA š°š°ā¦.MASHABIKI MUOMBEENI TUā¦.LA SIVYO MHHHHā¦. appeared first on Soka La Bongo.






Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!