Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

SIRI YAFICHUKA SIMBA KUKOSA MATOKEO, MAGORI

  • 128
Scroll Down To Discover

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba, Crescentius Magori, ameweka wazi sababu kuu zinazosababisha timu hiyo kupata matokeo yasiyoridhisha katika baadhi ya mechi za hivi karibuni.

Magori amesema  majeraha ya wachezaji muhimu yamekuwa kikwazo kikubwa kwa kikosi hicho, hali inayomfanya kocha kushindwa kutumia nguvu kamili ya timu katika kila mchezo.

Amesisitiza kuwa hakuna kiongozi wa klabu anayeweza au anayeshawishi wachezaji kucheza chini ya kiwango chao kwa makusudi ili timu ipate matokeo mabovu, akieleza kuwa madai hayo hayana ukweli wowote.

Kwa mujibu wa Magori, changamoto ya majeraha imeikumba Simba katika kipindi ambacho timu ilikuwa katika mchakato wa mpito wa mabadiliko ya benchi la ufundi, jambo lililoathiri uimara wa kikosi.

Ameeleza kuwa kocha mmoja alianza kujenga timu kutoka chini, lakini akaondoka, akaja kocha mwingine naye akaondoka, huku baadhi ya wachezaji muhimu wakiwa nje ya uwanja kutokana na majeraha ya muda mrefu.

“Sio kweli kwamba viongozi wanawaambia wachezaji wacheze chini ya kiwango. Kifundi tumepata shida kwa sababu ya mabadiliko ya makocha na pia majeraha ya wachezaji wetu muhimu,” amesema Magori.

Amesema   hakuna mchezaji anayelipwa vizuri na klabu kwa lengo la kuipiga Simba, wala hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kumshawishi mchezaji acheze chini ya kiwango chake kwa maslahi binafsi.

The post SIRI YAFICHUKA SIMBA KUKOSA MATOKEO, MAGORI appeared first on Soka La Bongo.



Prev Post HERSI AIBUA DIRA YA SOKA LA AFRIKA
Next Post Polisi Wakana Taarifa za Gari la Polisi Kusababisha Kifo cha Mwananchi Kongowe – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook