Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

DRC na Waasi wa M23 Watia Saini Makubaliano ya Amani Nchini Qatar

  • 14
Scroll Down To Discover

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kundi la waasi la M23 wametia saini makubaliano mapya ya mpango wa amani yanayolenga kusitisha mapigano na kurejesha utulivu katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo.

Hafla ya utiaji saini ilifanyika leo mjini Doha, Qatar, ikihudhuriwa na wawakilishi wa pande zote mbili pamoja na wapatanishi kutoka Qatar, Marekani na Umoja wa Afrika. Nchi hizo zimekuwa zikiongoza mazungumzo ya muda mrefu yaliyolenga kumaliza mzozo unaoendelea katika eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.

Kwa miezi ya karibuni, M23 imeendelea kupata ushindi katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ikiwa ni pamoja na kuteka Jiji la Goma mwezi Januari — jiji kubwa na muhimu zaidi Mashariki mwa DRC. Tangu kurejea katika mapigano mwishoni mwa 2021, kundi hilo limefanikiwa kudhibiti maeneo mengi kwa msaada ambao serikali ya DRC imekuwa ikiutaja kutoka nchini Rwanda, hatua iliyochochea ongezeko la mgogoro wa kibinadamu.

Akizungumzia makubaliano hayo, msuluhishi mkuu wa Qatar, Mohammed Al-Khulaifi, alisema kuwa yanaashiria hatua ya kihistoria katika safari ya kurejesha amani. Aliongeza kuwa juhudi za upatanishi zitaendelea hadi amani ya kudumu ipatikane katika maeneo yote yaliyoathirika.

SAUDI ARABIA YAJENGA UWANJA wa MPIRA ANGANI – UNA VITUO vya BURUDANI na MAZOEZI…



Prev Post Makamu wa Rais Nchimbi Amwakilisha Rais Samia Katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa ICGLR Nchini DRC
Next Post Jasinta Makwabe Atoa Neno La Nguvu Kwa Mabinti Wa Chuo Cha Urembo
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook