Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mtoto Miaka 3 Wa Askari Magereza Afariki Dunia Kwa Kusombwa Na Maji Mtoni – Video

  • 28
Scroll Down To Discover

Mtoto wa kiume, Samiu Salim, mwenye umri wa miaka mitatu na nusu, amefariki dunia baada ya kuzama kwenye maji ya Mto Faeli katika mtaa wa Mruki, mjini Babati, mkoa wa Manyara. Tukio hilo limetokea Aprili 19, 2025, majira ya saa 9 alasiri.

Kwa mujibu wa mashuhuda, mtoto huyo alikuwa na baba yake ambaye alikuwa akifanya shughuli zake kandokando ya mto huo. Hata hivyo, baada ya kumaliza shughuli zake, baba huyo hakumuona tena mtoto wake na alikuta viatu vya plastiki (yebo yebo) katika eneo alilomuacha. Hapo ndipo alipotambua kuwa mtoto alikuwa tayari amezama mtoni.

Baada ya juhudi za uokoaji, mwili wa mtoto ulipatikana umbali kidogo kutoka alipozamia, akiwa tayari amefariki dunia.



Prev Post Mama wa Kizungu Amlilia Rais Samia Adai Kunyanyaswa Kesi Yakwama Polisi Miezi 6 Bila Hatua- Video
Next Post Chama cha Kabila chasimamishwa DRC baada ya mali zake kuvamiwa
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook