Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Waziri Mkuu Majaliwa, Makamu Wa Rais Dkt. Mpango Wahudhuria Ibada Ya Kumuombea Mwalimu Nyerere Mbeya

  • 6
Scroll Down To Discover

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ameshiriki leo, Oktoba 14, 2025, katika Ibada ya kumuombea Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Francisko wa Asizi, Mwanjelwa, Mkoani Mbeya.

Makamu wa Rais, Dkt. Philip Isdor Mpango, pia alihudhuria ibada hiyo, ikionesha mshikamano wa viongozi wa nchi katika kumbukumbu za Baba wa Taifa.

Ibada hiyo imeongozwa na Akofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbeya, Mhashamu Gervas Nyaisonga, huku wakiombea amani, mshikamano wa taifa, na baraka kwa wananchi wa Tanzania.

Tukio hilo limekuwa fursa kwa viongozi na wananchi kuenzi urithi wa uongozi wa Hayati Mwalimu Nyerere, akisisitiza maadili ya mshikamano, utu, na maendeleo ya taifa.



Prev Post Kanisa Katoliki Wakanusha Waraka wa Uchaguzi “Ni FAKE!” – Video
Next Post Rais wa Madagascar Andry Rajoelina Ajificha Baada ya Jaribio la Kumuua
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook