Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Raila Odinga Amkosoa Rais Ruto Agizo la Kuwapiga Risasi Waandamanaji

  • 37
Scroll Down To Discover

Aliyekuwa Waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani wa muda mrefu, Raila Odinga

Nairobi, Kenya – Aliyekuwa Waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani wa muda mrefu, Raila Odinga, amemkosoa vikali Rais William Ruto kufuatia agizo lake la kuwaruhusu maafisa wa polisi kutumia nguvu, ikiwemo kuwapiga risasi miguuni waandamanaji waliohusika kwenye maandamano ya hivi karibuni.

Kupitia taarifa rasmi aliyoitoa Ijumaa, Julai 11, 2025, Raila alieleza kuwa agizo la kuwafyatulia risasi raia hata wale wanaodaiwa kuvunja sheria ni kinyume cha sheria, haki za binadamu, na misingi ya utawala wa kisheria.

“Katika maandamano au mazingira yoyote yanayohitaji utekelezaji wa sheria, maagizo ya kuwapiga risasi, kuwalemaza, au hata kuwasumbua raia ni makosa,” alisema Raila.

Raila, ambaye ni mmoja wa viongozi walioungana na serikali pana ya Ruto kupitia muungano wa kitaifa, alisisitiza kuwa utawala wa sheria ndio njia pekee ya kushughulikia raia wanaokiuka sheria, na sio matumizi ya nguvu kupita kiasi au hukumu za papo kwa papo.

Kauli hiyo ya Raila inakuja baada ya Rais Ruto, mnamo Jumatano, Julai 9, kutoa matamshi makali akiwatuhumu watu aliodai wanafadhili maandamano ya vurugu kwa lengo la “kubadilisha serikali kwa njia zisizo za kikatiba.” Katika hotuba hiyo, Ruto alionyesha hasira, akisema serikali yake haitakubali taifa kuyumbishwa.

“Nimekuwa nikivumilia, lakini sasa inatosha. Serikali haitavumilia njama za kuvuruga nchi,” alisema Rais Ruto.

Hata hivyo, Raila alitoa wito kwa serikali kufuata taratibu za kisheria, kuhakikisha wahalifu wanakamatwa na kufikishwa mahakamani badala ya kupigwa risasi.

“Ni lazima tuhifadhi utu wa kila Mkenya na kulinda haki za binadamu. Polisi wanapaswa kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria, si vinginevyo,” alisisitiza.

MAAMUZI ya MAHAKAMA JUU ya KANISA la GWAJIMA LEO – WAUMINI WAKUSANYIKA NJE ya MAHAKAMA KUU…



Prev Post Wachumba Waliotrendi, Mrefu Na Mfupi Watangaza Ndoa Ya Kihistoria – Video
Next Post Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango Afungua Mkutano wa Mwaka wa Waganga Wakuu Dodoma
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook