Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Fatma Ferej Ateuliwa Rasmi Mgombea Mwenza wa Urais ACT Wazalendo

  • 45
Scroll Down To Discover

Katibu wa Ngome ya Wanawake ya ACT Wazalendo, Fatma Abdulhabib Ferej

Katibu wa Ngome ya Wanawake ya ACT Wazalendo, Fatma Abdulhabib Ferej, ameteuliwa rasmi kuwa mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya jina lake kupitishwa kwa kauli moja na Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho uliofanyika mkoani Dar es Salaam.

Uteuzi wa Ferej ulitangazwa rasmi usiku wa manane wa siku ya Alhamisi na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu, ambaye aliwasilisha jina hilo mbele ya mkutano kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya chama.

Baada ya utangazaji huo, Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo (Bara), Isihaka Mchinjita, aliwahoji wajumbe wa Mkutano Mkuu kuhusu uamuzi wa uteuzi huo, ambapo wote waliitikia kwa sauti ya pamoja, “Ndiyo!”, kuashiria kuidhinishwa rasmi kwa jina hilo.

Ferej ni mwanasiasa nguli kutoka visiwani Zanzibar, mwenye rekodi ya uongozi na ushujaa katika masuala ya kijamii na kisiasa. Mwaka 2013, alitunukiwa Tuzo ya Mwanamke Jasiri na Serikali ya Marekani kupitia ubalozi wake nchini Tanzania.

Kwa uteuzi huu, Ferej atakuwa mgombea mwenza wa Luhaga Mpina, ambaye naye alipitishwa kuwa mgombea Urais kupitia chama hicho kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.



Prev Post Bei ya Mafuta Yapungua Dar, Yapanda Mtwara – EWURA Yatangaza Bei Mpya za Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa
Next Post Mechi Tatu, Mkeka Mmoja – Ushindi Mkubwa Unakungoja Meridianbet
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook