Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mtoto wa Mzee Samatta Azungumzia Chanzo cha Kifo cha Baba Yao – Video

  • 52
Scroll Down To Discover

Rajab Ally Samatta, mtoto wa kwanza wa marehemu Mzee Ally Samatta

Rajab Ally Samatta, mtoto wa kwanza wa marehemu Mzee Ally Samatta, ambaye ni baba mzazi wa mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta , amefunguka kuhusu chanzo cha kifo cha baba yao kilichotokea mapema leo katika Hospitali ya Kilwa Road jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Global TV, Rajab ambaye pia ni msemaji wa familia, amesema kuwa marehemu baba yao alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu, hali iliyosababisha changamoto za kiafya zilizompelekea kufariki dunia.

“Ni kweli baba yetu amefariki leo asubuhi. Amekuwa akisumbuliwa na kisukari kwa muda mrefu, na leo hali yake ilizidi kuwa mbaya akiwa hospitalini,” amesema Rajab kwa huzuni.

Taarifa zaidi kuhusu ratiba ya mazishi na shughuli nyingine za msiba zitatolewa na familia kadri mipango inavyoendelea.

Watu mbalimbali, wakiwemo mashabiki wa soka, viongozi wa michezo, wasanii, na wananchi kwa ujumla, wameendelea kuonesha mshikamano na kutoa pole kwa familia ya Samatta kupitia mitandao ya kijamii.



Prev Post Tantrade Yaadhimisha Programu ya Urithi Wetu kwa Kuwakutanisha Wanafunzi
Next Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 07, 2025.
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook