
MAGAZETI ya Leo Jumapili 08 June 2025
MAGAZETI ya Leo Jumapili 08 June 2025
Wakati Serikali ikitangaza kuufungia mtandao wa X (twitter zamani) hapa nchini wafanyabiashara na wahamasishaji (infulencers) wameanza kuonja joto la jiwe.
Hiyo ni baada ya biashara zilizokuwa zikifanyika katika mtandao huo kuanza kudorora huku baadhi ya kampuni zikisitisha mikataba waliyokuwa wameingia na watumiaji mbalimbali wa mtandao huo ikiwemo zile zilizohusu kampeni mbalimbali.
Hivi karibuni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa kuweka wazi kuwa iwapo mwananchi anashindwa kupata mtandao fulani ajue kuwa Serikali imefanya namna kumlinda Mtanzania.
“Kama umeona kuna baadhi ya mtandao siyo lazima uwe X wowote hata YouTube kuna kitu unatafuta hukipati ujue ni kazi inayofanywa na Serikali kuhakikisha inamlinda mlaji na kuhakikisha watu wote wanaoendesha huduma kwenye anga la Taifa letu wanafuata sheria,” amesema.
Silaa katika mahojiano yake na Kituo cha runinga cha Wasafi, alisema Kifungu cha 16 cha Kanuni ya Maudhui ya Mtandao ya mwaka 2000, kinaeleza aina ya maudhui yanayopaswa kuchapishwa katika mtandao husika.
Licha ya kutokuwa tayari kutaja majina yao lakini walilaani kitendo hicho huku wakieleza kuwa kinawarudisha nyuma kiuchumi kwani mtandao huo ulikuwa sehemu ya mapato wanayoyategemea kila mwezi.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!