
Nilipata kazi yangu ya ndoto baada ya kungoja kwa muda mrefu. Nilijua itakuwa nafasi ya kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Hata hivyo, mambo hayakuenda vile nilivyotarajia.
Baada ya miezi michache nilianza kugundua bosi wangu hakuwa akinipenda. Alionekana kunionea wivu kwa jinsi nilivyokuwa nafanya kazi vizuri na nilipata sifa kutoka kwa wafanyakazi wenzangu.
Kila mradi nilipewa nilifanya kwa bidii, lakini kila mara alitafuta kosa dogo la kunilaumu mbele ya wenzangu. Aliniweka kwenye shinikizo kubwa na aliniandikia barua ya onyo mara mbili kwa sababu ambazo hazikuwa na msingi. Nilihisi kama alitaka niachishwe kazi. Wafanyakazi wenzangu walinionea huruma lakini hakuna aliyethubutu kumkabili.SOMA ZAIDI
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!