Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Benki ya Exim Ikishirikiana na Mind Matters Yaunga Mkono Mafanikio ya Wanawake Kupitia Mafunzo ya ‘Mindful Leadership’

  • 4
Scroll Down To Discover

Benki ya Exim Tanzania, kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi Wanawake (Women Empowerment Program – WEP) chini ya ‘Exim Cares’, imejitokeza kama Mdhamini Mkuu wa Mafunzo ya ‘Mindful Leadership Training for Women’. Mafunzo haya yanawaleta pamoja viongozi zaidi ya 150 wa kike kutoka sekta mbalimbali za biashara, elimu, na sekta za umma, huku yakilenga kuimarisha uongozi wa kina, akili ya hisia, ustahimilivu, na ubunifu.

Mafunzo haya yatatolewa katika awamu tatu: 27 Septemba, 4 Oktoba, na 11 Oktoba 2025. Kila darasa litahusisha mafunzo ya mazoezi ya vitendo, huku washiriki wakipata nafasi ya kubadilishana mawazo na kupewa uizoefu kutoka kwa wataalam wa uongozi.

Akizungumza kuhusu mpango huu, Mkuu wa Idara ya Masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Stanley Kafu, alisema, “Tunafurahia kushirikiana na Mind Matters katika mpango huu muhimu unaolenga kukuza uongozi wa wanawake. Kupitia WEP, tunatoa fursa kwa wanawake kupata ujuzi wa ujasiriamali, ustahimilivu, na uwezo wa kuongoza hisia binafsi, jambo linalowasaidia kustawisha maisha yao, familia zao, na jamii zao kwa ujumla.”

Meneja Mkuu wa Masoko na Mwasiliano wa Benki ya Exim Kauthar D’souza, aliongeza,
“Usambazaji wa ujuzi huu ni kielelezo cha jitihada zetu za kudumisha usawa wa jinsia na kuwekeza katika wanawake ili waanzishe mabadiliko chanya. Mpango huu unaungana moja kwa moja na mradi wa WEP unaolenga kuendeleza ujasiriamali, kuimarisha uwezo, na kutoa fursa sawa kwa wanawake katika kila nyanja ya maisha. Na ndio maana tukaamua kuungana nao”

Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Kauthar D’souza akizungumza na wanawake waliojiunga na mafunzo ya ‘Mindful leadership’ kwa ushirikiano na Mind Matters yenye lengo la kuwaendeleza wanawake katika ujasiriamali , kuimarisha uwezo, na kutoa fursa sawa kwa wanawake kwenye kila nyanja za maisha. Mafunzo haya yatakua na jumla ya awamu tatu, yakilenga kuwanufaisha wanawake 150. Tukio hili limefanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi wa Mind Matters Nadia Ahmed alisema, “Tunashukuru sana kwa ushirikiano huu na Benki ya Exim. Mafunzo ya ‘Mindful Leadership’ ni zaidi ya kujenga uongozi; ni kubadilisha maisha ya wanawake, kuongeza ustahimilivu wao, na kuimarisha jamii zao. Ushirikiano huu unaleta thamani ya moja kwa moja kwa wanawake zaidi ya 150, na ni hatua kubwa katika kuendeleza uongozi wa wanawake Tanzania.”

Mafunzo haya ya ‘Mindful Leadership’ yanaunga mkono wa juhudi za Exim Bank za kudumisha mpango wa WEP uliopangwa kwa muda mrefu, ambapo lengo ni kuifikia idadi kubwa ya wanawake zaidi ya 600,000 ifikapo mwaka 2028. Programu hii inajumuisha mafunzo, mikutano, uwezo wa kuongoza hisia binafsi, na mitandao ya kibiashara ili kuhakikisha wanawake wanapata motisha, ujuzi, na rasilimali zinazohitajika kufanikisha maisha yao binafsi na ya jamii kwa ujumla.

Kwa kuwekeza katika mpango huu, Exim Bank inathibitisha nafasi yake kama kiongozi wa kuunga mkono uwezeshaji wa wanawake na maendeleo endelevu, huku ikichangia moja kwa moja katika maendeleo ya jamii na uchumi wa Tanzania. Ushirikiano huu wa kimkakati unaendana na malengo ya Exim Bank ya kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi, sambamba na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

The post Benki ya Exim Ikishirikiana na Mind Matters Yaunga Mkono Mafanikio ya Wanawake Kupitia Mafunzo ya ‘Mindful Leadership’ appeared first on SwahiliTimes.



Prev Post Vodacom Tanzania Foundation na JKCI Washirikiana Kupanua Huduma za Moyo kwa Watoto
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook