
MAGAZETI ya Leo Jumapili tarehe 22 June 2025
MAGAZETI ya Leo Jumapili tarehe 22 June 2025
Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars’ imetwaa ubingwa wa mashindano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kenya.
Bao pekee la ushindi la Twiga Stars lilikuwa la kujifunga la Enez Mango wa Kenya katika dakika ya 49 aliyekuwa katika harakati za kuokoa hatari langoni mwake.
Ushindi huo umeifanya Twiga Stars ifikishe pointi 12 katika mechi nne ilizocheza na hivyo kujihakikishia taji huku Kenya ikimaliza katika nafasi ya pili na Uganda ipo nafasi ya tatu.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!