Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Waziri Mkuu Awataka Wana-Lindi Kumchagua Dkt. Samia Oktoba 29

  • 9
Scroll Down To Discover

LINDI-Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Wana-Lindi wanakila sababu ya kumchagua Dkt.Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,mwaka huu.

Amesema kuwa,Rais Dkt.Samia amegusa matamanio ya Wana-Lindi kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo kwa kiasi kikubwa imegusa maisha ya kila siku ya wakazi wa mkoa huo.

Amesema hayo Septemba 13,2025 katika uzinduzi wa kampeni za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Lindi na Wilaya ya Ruangwa zilizofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Likangala, Ruangwa mkoani Lindi.

“Tunayo sababu ya kuwachagua wagombea wa Chama cha Mapinduzi, sote tunafahamu namna Rais Dkt.Samia alivyotekeleza miradi katika mkoa huu, kwenye sekta za elimu, afya, maji, barabara, uwezeshaji wananchi kiuchumi. Mkoa huu tunamiradi mikubwa itakayoufanya uchangamke na kuchachua uchumi wetu.”

 



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 15, 2025
Next Post Burkina Faso Yapunguza Sikukuu za Umma Kuokoa Bilioni 17
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook