Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Kikwete, Ramaphosa na Boko Wapanga Mwelekeo Mpya wa Uwekezaji wa Maji Afrika

  • 3
Scroll Down To Discover

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa (kulia) na Rais wa Botswana Mhe. Duma Boko kabla ya kuanza Mkutano wa Kwanza wa Uwekezaji wa Maji Afrika jijini Cape Town, Afrika Kusini, ulioitishwa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini pamoja na Jopo la Ngazi ya Juu la Programu ya Uwekezaji wa Maji Afrika (Africa Water Investment Programme – AIP).

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameungana na Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa, na Rais wa Botswana, Mhe. Duma Boko, katika Mkutano wa Kwanza wa Uwekezaji wa Maji Afrika uliofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini.

Mkutano huo, ulioratibiwa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini na Jopo la Ngazi ya Juu la Programu ya Uwekezaji wa Maji Afrika (Africa Water Investment Programme – AIP), umebeba dhamira ya kuhamasisha na kuongeza uwekezaji mkubwa katika sekta ya maji barani Afrika.

Viongozi hao watatu, pamoja na wakuu wengine wa nchi, mawaziri, wawekezaji na wadau wa maendeleo, wanajadili mbinu na sera za kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji safi na salama, kuongeza miundombinu ya maji, pamoja na kulinda vyanzo vya maji ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji inayoikabili Afrika.

Kwa mujibu wa waandaaji, mkutano huu ni hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa miradi mikubwa ya maji inayolenga kufanikisha ajenda za maendeleo endelevu, kukuza uchumi wa kijani na kuboresha maisha ya wananchi barani kote.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini na Mfalme Mswati III wa Eswatini katika Mkutano wa Kwanza wa Uwekezaji wa Maji Afrika jijini Cape Town, Afrika Kusini, ulioitishwa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini pamoja na Jopo la Ngazi ya Juu la Programu ya Uwekezaji wa Maji Afrika (Africa Water Investment Programme – AIP).

 



Prev Post Jela Maisha Kwa Kumlawiti Mtoto Wa Miaka 4
Next Post Bwawa la Ethiopia Latishia Usalama wa Maji Misri
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook