Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

WAZIRI JAFO APONGEZA DIB KWA KUCHANGIA UTULIVU WA SEKTA YA FEDHA

  • 50
Scroll Down To Discover

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo (Kulia), akipokea zawadi kutoka kwa Isack Kihwili Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Bima ya Amana wakati alipotembelea katika banda la bodi hiyo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Saba Saba  yanayoendelea kwenye viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar er Salaam.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo, akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea katika  banda la Bodi ya Bima ya Amana kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba yanayoendelea kwenye viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar er Salaam.

………

Na John Bukuku, Dar es Salaam

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo, ametembelea banda la Bodi ya Bima ya Amana (DIB) na kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na bodi hiyo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Dkt. Jafo alipata maelezo ya kina kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na DIB kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Bw. Isack Kihwili.

Waziri huyo alipongeza kazi nzuri inayofanywa na DIB, hususan katika kuhakikisha utulivu wa sekta ya fedha kupitia ulinzi wa amana za wananchi katika taasisi za fedha.

 “Niwahimize wananchi kuendelea kutumia huduma za kibenki kwa kujiamini, wakifahamu kuwa amana zao zinalindwa kupitia Bodi ya Bima ya Amana. Huu ni mfumo muhimu sana kwa usalama wa fedha na ustawi wa uchumi wetu,” alisema Dkt. Jafo. 

DIB ina jukumu la kulinda amana za wateja wa taasisi za fedha zilizosajiliwa, na hivyo kuongeza imani kwa wananchi kutumia huduma za kifedha kwa usalama zaidi.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JULAI 11, 2025
Next Post JIPATIE SPIN ZA BURE KILA SIKU KWENYE WILD WHITE WHALE NA MERIDIANBET…
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook