Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Kesi ya Tundu Lissu: EU Yatoa Wito wa Uangalizi wa Kimataifa

  • 26
Scroll Down To Discover

Bunge la Ulaya limetoa maazimio kadhaa kwa Tanzania kuhusu sakata la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu ambapo limeitaka serikali kumuachia huru mara moja bila masharti na kuhakikisha usalama wake.

Pia limezitaka mamlaka za Tanzania kusitisha kukamatwa kiholela kwa wapinzani, vitendo vya vurugu, mashambulizi na unyanyasaji dhidi ya wanachama wa upinzani, watetezi wa haki za binadamu, wanahabari na mashirika ya kiraia.

Pia limezitaka mamlaka hizo kuchunguza kwa uhuru ukiukwaji unaodaiwa kufanywa na polisi pamoja na matukio ya kutoweka kwa watu.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu.

Pia limeitaka serikali kurekebisha sheria zake za makosa ya mtandaoni na za vyombo vya habari kuendana na sheria za kimataifa za haki za binadamu.

Pia limezitaka mamlaka za Tanzania kuirudisha Chadema kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Oktoba 2025 na kushirikiana na vyama vyote vya siasa.

Pia limeutaka Umoja wa Ulaya (EU) na nchi wanachama wake kushirikiana kwa makini na mamlaka za Tanzania kuhusu kesi ya Lissu na kufuatilia kwa karibu mwenendo wa kesi hiyo.



Prev Post Rais Samia Ampokea Rais Wa Jamhuri Ya Msumbiji Ikulu Dar – (Picha +Video)
Next Post Waziri Kombo: Hakuna Sheria Iliyovunjwa Katika Utendaji wa Serikali
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook