Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

DEPU BADO ANA SAFARI NDEFU, PEDRO

  • 19
Scroll Down To Discover

KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amefunguka kuhusu mshambuliaji wao Laurindo Dilson Maria Aurélio maarufu kama Depu, akisema licha ya kuonyesha uwezo mkubwa uwanjani bado ana mengi ya kujifunza ili kufikia kiwango chake cha juu.

Pedro amesema Depu ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa, lakini bado anakumbana na changamoto ndogo ndogo za kiufundi na kimbinu zinazomzuia kuonyesha uwezo wake wote kwa ukamilifu ndani ya uwanja.

Kocha huyo raia wa Ureno ameeleza kuwa jukumu la benchi la ufundi ni kufanya kazi kwa karibu na mshambuliaji huyo ili kumsaidia kuboresha maeneo anayohitaji marekebisho na hatimaye kufikia ubora anaoutamani.

“Depu ana nguvu, kasi na uwezo mkubwa wa kufunga mabao, lakini bado anahitaji utulivu zaidi anapopata nafasi za wazi ili kuzitumia kwa manufaa ya timu,” amesema Pedro.

Ameongeza kuwa Depu ni miongoni mwa wachezaji wanaojituma kwa kiwango kikubwa mazoezini na ana kiu ya mafanikio, hali inayompa matumaini makubwa kuwa atakuwa silaha muhimu kwa Yanga katika michezo ijayo.

Pedro pia amewaomba mashabiki wa Yanga kuwa wavumilivu kwa mshambuliaji huyo, akisisitiza kuwa maendeleo ya mchezaji ni mchakato unaohitaji muda, imani na sapoti kutoka kwa kila mmoja ndani na nje ya uwanja

The post DEPU BADO ANA SAFARI NDEFU, PEDRO appeared first on Soka La Bongo.



Prev Post BUBA KULIA, NZENGELI KUSHOTO YANGA YA MOTO
Next Post NINA DENI KWA WANA SIMBA, KIBABAGE
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook