Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mahakama ya Uturuki yatoa vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na waziri wake

  • 14
Scroll Down To Discover

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu

Mamlaka ya mahakama nchini Uturuki imetoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, Waziri wake wa Ulinzi, na maafisa wengine 35 wakuu wa jeshi na serikali ya Israel, wakikabiliwa na tuhuma za uhalifu wa kivita na mauaji ya kimbari.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Istanbul, uamuzi huo unahusiana na vitendo vya kijeshi vya Israel katika Ukanda wa Gaza na dhidi ya kundi la kimataifa lililokuwa likijaribu kutoa misaada ya kibinadamu kwa Wapalestina waliokuwa wamezingirwa.

Israel, kupitia msemaji wake wa serikali, imekanusha vikali tuhuma hizo, ikisema kuwa inaendesha vita dhidi ya ugaidi, si dhidi ya raia wa Palestina.

Hatua hii ya kiishara kutoka kwa Uturuki imekuja wakati Marekani ikiendelea kukiri nafasi muhimu ya Ankara katika juhudi za kimataifa za kuwapokonya silaha Hamas na kushirikiana katika kikosi cha amani cha kimataifa kinacholenga kutekeleza mpango wa amani wa Donald Trump kwa Gaza.

Ripoti zinaeleza kuwa uamuzi wa mahakama hiyo umetolewa ndani ya mfumo maalum wa uchunguzi wa uhalifu wa kivita, unaolenga kuchunguza mashambulizi ya Israel dhidi ya raia, hospitali na misafara ya misaada, ikiwemo “Global Solidarity Convoy” iliyoshambuliwa huko Gaza.

Wachambuzi wa siasa za kimataifa wanasema, ingawa hati hiyo haina nguvu za moja kwa moja nje ya mipaka ya Uturuki, ni ishara kali ya kisiasa inayoongeza shinikizo la kimataifa dhidi ya Israel kuhusu matendo yake ya kijeshi katika Gaza.

POLISI WANAMSAKA ASKOFU GWAJIMA – MNYIKA – LEMA na WENZAO 7 SAKATA la VURUGU SIKU ya UCHAGUZI MKUU..



Prev Post Vyuo Kufunguliwa Novemba 17, Wizara Yatoa Ratiba Mpya ya Masomo 2025/26
Next Post Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Amani Golugwa Akamatwa Arusha
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook