Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia Apokea Ujumbe Maalum Kutoka kwa Rais wa DRC

  • 20
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Congo (DRC) Felix Antoine Tshisekedi, uliowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa nchi hiyo, Floribert Anzuluni, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 24 Oktoba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Felix Antoine Tshisekedi.

Ujumbe huo uliwasilishwa kwa Rais Samia na Mjumbe Maalum ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa DRC, Floribert Anzuluni, katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalihusu kuimarisha ushirikiano wa kijamii, kiuchumi, na kidiplomasia kati ya Tanzania na DRC, hususan katika maeneo ya biashara, usafirishaji, na amani ya kikanda.

Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizo mbili na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kukuza maendeleo ya wananchi wa Tanzania na DRC.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 26, 2025
Next Post Dkt. Samia Azungumza na Ujumbe wa Uangalizi wa Uchaguzi wa AU
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook