Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Bodaboda, Wamachinga, na Walemavu Wagomea Maandamano ya Aprili 24

  • 10
Scroll Down To Discover

Saidi Kagomba Mwenyekiti wa Shirikisho la Waendesha Bodaboda na Bajaj (kushoto) akizungumzia tukio hili.
Umoja wa Maafisa Usafishaji maarufu kama waendesha Bodaboda na Bajaj, Umoja wa Wamachinga na Wenye Uhitaji maalum (Walemavu) wote kwa pamoja leo wametangaza kuyagomea maandamano yaliyohamasishwa na chama cha Demokrasia na Maendeleo ‘CHADEMA’ siku ya Aprili 24 mwaka huu.
Wote kwa pamoja wameyagomea maandamano hayo ya kukusanyika Mahakama ya Kisutu jijini Dar ambapo kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu itakuwa mahakamani hapo.
Wote kwa pamoja walidai wamechoka kutumiwa vibaya na wanasiasa ambao mwisho wa siku wakipatwa na matatizo wanatelekezwa.
Kwa upande wao Bodaboda wamekumbushia  mmoja wa viongozi wa CHADEMA alivyowahi kuwaambia kuwa  kazi yao ni ya laana. HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL 



Prev Post MAGAZETI ya Leo Jumanne 22 April 2025
Next Post Fahamu Mchakato Wa Kumchagua Papa Mpya Katika Kanisa Katoliki
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook