Waasi wa M23 katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wamesema hawatarudi katika mazungumzo ya amani huko Doha, Qatar, hadi pale serikali ya DRC itakapoheshimu kikamilifu misingi ya kumaliza vita. Msemaji wa kundi hilo, Lawrence Kanyuka, ameiambia BBC hii leo kwamba wawakilishi wa kundi hilo hawako Doha ambako mazungumzo yamepangwa kufanyika.
Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!