Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

WAZIRI KOMBO AMPOKEA RASMI WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA BIASHARA WA HUNGARY 

  • 2
Scroll Down To Discover

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amempokea rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Hungary, Mhe. Péter Szijjártó baada ya kuwasili katika Ofisi Ndogo za Wizara za jijini Dar es Salaam, Septemba 29, 2025.

Akiwa Wizarani hapo, Mhe. Szijjártó amekutana kwa mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake Mhe. Balozi Kombo yaliyofuatiwa na mazungumzo ya pande mbili ambayo yaliwashirikisha wajumbe mbalimbali kutoka Tanzania na Hungary wakiwemo Mawaziri.

Mhe. Szijjártó yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia baina ya Tanzania na Hungary.



Prev Post Netanyahu na Trump wakutana New York kuzungumzia suluhu ya Gaza
Next Post Mwili wa Hayati Askofu Mkuu Rugambwa wapokelewa Bukoba
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook