Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Dua Maalum ya Alhaj Omary Rashid Mchengerwa Yafanyika Rufiji, Pwani

  • 8
Scroll Down To Discover

Dua maalum ya kumbukumbu ya siku 40 tangu kufariki dunia kwa Alhaj Omary Rashid Mchengerwa imefanyika leo katika kijiji cha Ikwiriri, Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani.

Alhaj Omary Mchengerwa ni baba mzazi wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa, na alifariki dunia tarehe 24 Februari 2025 katika mji mtukufu wa Medina, Saudi Arabia.

Shughuli hii imewaleta pamoja ndugu, jamaa, marafiki, majirani, na viongozi mbalimbali waliokusanyika nyumbani kwa familia ya marehemu kwa ajili ya kumuombea dua.

Mgeni rasmi katika shughuli hiyo ya kiroho ni Mufti wa Tanzania, Sheikh Aboubakar bin Zuberi, ambaye amewaongoza waumini katika dua na mawaidha yenye mafunzo ya maisha na subira.

Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi. Amin.



Prev Post Rais Dkt. Samia Kufanya Ziara Ya Kiserikali Nchini Angola Kuanzia Aprili 7, 2025
Next Post Waziri Mkuu Kuongoza Harambee Ya Mei Mosi Kitaifa
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook