Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

MAGAZETI ya Leo Ijumaa 28 Machi 2025

  • 8
Scroll Down To Discover

MAGAZETI ya Leo Ijumaa 28 Machi 2025

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeanza rasmi upasuaji wa ubongo kwa kutumia ‘roboti’ (Akili Unde).

Upasuaji huo unahusisha kifaa kiitwacho ‘Brain Lab- Neuro Navigation System’ ambacho husaidia wataalamu kufanya upasuaji wa ubongo bila kufungua fuvu na kupunguza siku za mgonjwa kukaa wodini baada ya upasuaji huo.

Hayo yamesemwa Alhamisi Machi 27, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dk Mpoki Ulisubisya wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua hiyo.

“Kwa mara ya kwanza katika nchi yetu (Tanzania) leo tumefanikiwa kufanya upasuaji wa ubongo kwa kutumia kifaa maalumu ( Brain Lab- Neuronavigation System) ambacho kinamuongoza daktari mpaka kwenye shida ilipo bila kufungua fuvu wala mionzi ya X- Ray” amesema Dk Mpoki

Dk Mpoki amesema kuwa upasuaji huo umeongozwa na daktari bingwa mbobezi mzawa kwa kushirikiana na madaktari kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha nchini Marekani na kutoa wito kwa Watanzania wenye matatizo ya ubongo kufika katika taasisi hiyo kupatiwa matibabu.

Mkurugenzi wa upasuaji wa ubongo kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha nchini Marekani, Profesa Roger Hartl amewashukuru watumishi wa MOI kwa ushirikiano wao ambao wameendelea kumpatia tangia mwaka 2008 na ameahidi kuendelea kutembelea taasisi hiyo kwa ajili ya kuwapatia mafunzo na kuwajengea uwezo wataalam hao.



Prev Post MAGAZETI ya Leo Jumamosi 29 Machi 2025
Next Post Mr Blue na Lady Jaydee wametoa somo la Hip Pop
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook