
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imekubali maombi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu kujitetea mwenyewe katika kesi ya uhaini inayomkabili.
Lissu anayewakilishwa na Jopo la Mawakili zaidi ya 30, aliwasilisha maombi hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Franko Kiswaga baada ya Jopo la Mawakili wanaomtetea kujitambulisha.
Baada ya kuwasilisha maombi hayo, Hakimu Kiswaga alisema anakubaliana na maombi hayo hivyo Lissu atajitetea mwenyewe hadi pale atakaposema basi.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!